Lyrics

Mbosso – Amepotea Lyrics

Here are the lyrics to the song “Amepotea” by Mbosso:

VERSE 1 

Vipeperushi vinasambaa 

Eti natafutwa nimepotea

Wiki imekata 

Ndugu wamechachamaa 

Wananitafuta mwezi umekataa 

BRIDGE 

Kazini sionekani 

Yupo wapi huyu simuni 

Sipatikani 

Yupo wapi huyu 

Baba kaniulizia 

Yupo wapi huyu 

Mama ahisi kulia 

Yupo wapi huyu 

CHORUS 

Mimi nimezamaaa 

Katika kina kirefu 

Cha bahari ya mapenzi 

Nimezama katika kina kirefu 

Cha bahari ya mapenzi 

VERSE 2 

Siwe handiti pule mwanarajabu

Mliomkuta Tanga 

Sijafanywa msukule 

Msipate taabu 

Kumaliza waganga 

Amenirudisha shule 

Hesabu maumbo kupanga 

Penzi la wasasambule 

Lenye protini vitamini na wanga 

Ooh oooh ooooh 

Ladha yake si sukari

Ni vichenza na malimau 

Mechi zake huwa hatari 

Ni chenga na mambao 

BRIDGE 

Kazini sionekani 

Yupo wapi huyu simuni 

Sipatikani 

Yupo wapi huyu 

Baba kaniulizia 

Yupo wapi huyu 

Mama ahisi kulia 

Yupo wapi huyu 

CHORUS 

Mimi nimezamaaa 

Katika kina kirefu 

Cha bahari ya mapenzi 

Nimezama katika kina kirefu 

Cha bahari ya mapenzi

Mbosso – Amepotea Mp3 Download

Telegram
Shares: